(Katekisimu Ndogo ya Westminster, asili ya mwaka 1647).
Mwaka 1643, Bunge la Muda Mrefu la Uingereza lilipoliita Mkutano wa Westminster kutoa Ungamo la Imani, na pia likaweka mwelekeo wa "Katekisimu". Mkutano ulimwomba Herbert Palmer kuunda mswada wa Katekisimu, lakini Robert Baillie na wajumbe wengine wa Uskoti walivunjika moyo. Mwezi Desemba iliwekwa kamati ya kuandika katekisimu na Januari 1647, Mkutano uliacha kuandika katekisimu moja na kuigawanya katika mbili: Katekisimu Ndogo, ambayo ingekuwa ya "kusoma kwa urahisi na kwa ufupi, kwa ajili ya wanaoanza" na Katekisimu Kubwa, yenye usahihi zaidi na inayoeleweka zaidi.
Katekisimu ilikamilishwa mwaka 1647 na mwaka uliofuata ikakubaliwa na Mkutano Mkuu wa Uskoti.